Psalms 2:1-5

Mfalme Aliyechaguliwa Na Mungu

1 aKwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya,
na kabila za watu kula njama bure?
2 b cWafalme wa dunia wanajipanga
na watawala wanajikusanya pamoja
dhidi ya Bwana
na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 dWanasema, “Tuvunje minyororo yao
na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”

4 eYeye atawalaye mbinguni hucheka,
Bwana huwadharau.
5 fKisha huwakemea katika hasira yake
na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
Copyright information for SwhNEN